Ratiba ya Copa America Centenario 2016, kuanza Juni, USA
Michuano ya mataifa ya Marekani ya Kusini yatakayo fanyika huko USA yakiwa ni Mashindano maalum ya kusheherekea Miaka 100 na kujumuisha Nchi 16 zikiwemo Nchi waalikwa wakiwemo wenyeji USA na hii ndo Droo ya kupanga Makundi.
Makundi Manne yenye Timu 4 kila moja yamepangwa na Mabingwa Watetezi Chile wapo Kundi D pamoja na Argentina, Panama na Bolivia.
Michuano hii itachezwa kwenye Viwanja 10 vinavyo chukua washabiki zaidi ya 50,000 kila kimoja ambavyo ni Santa Clara, Seattle, Pasadena, Glendale, Houston, Chicago, Philadelphia, East Rutherford, Foxborough na Orlando.
Wenyeji USA, ambao wapo Kundi A, watafungua dimba Juni 3 kwa kucheza na Colombia huko Santa Clara, California.
Na fainali itachezwa Juni 26 ndani ya uwanja wa MetLife Stadium, East Rutherford.