Burudani

Ray C afunguka ujio wa albamu na jinsi Diamond alivyoamua kumbeba (Video)

Msanii mkongwe wa muziki, Rehema Chalamila aka Ray C amefunguka kuhusu ujio wake mpya baada ya misukosuko ya maisha pamoja na ishu ya kusaini, Wasafi.Com ya Diamond Platnumz.

Muimbaji huyo ambaye ana mashabiki wengi amepambana kwa muda mrefu kutoka katika matumizi ya dawa za kulevya ambayo yalimsumbua kwa muda mrefu.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii akiwa mwenye siha njema na muonekano wa kuvutia, Ray C amedai kwa sasa amerudi upya kwenye muziki akiwa amejipanga na kazi nyingi pamoja albamu mpya.

“Kazi nimeanza upya natengeneza albamu, mpaka sasa hivi na nyimbo kama kumi,” alisema Ray C. “Nimependa kwa sababu nimekaa muda mrefu kimya bila kutoa kazi yoyote kwahiyo hiyo ni kama zawadi kwa mashabiki wangu. Lakini pia tumeanza na wimbo ‘Unanimaliza’ na umepokelewa vizuri sana na mashabiki na kuna mambo ya video yanakuja yaani ni back to back huu mwaka ni kwaajili kazi,”

Muimbaji huyo alisema amesaini mkataba mpya na Wasafi.Com kwaajili ya kumsambazia kazi zake mpya za muziki.

“Kuhumu ukaribu wangu na Diamond ni kwa sababu tuna mahusiano ya kikazi. Wasafi.Com iko chini ya Diamond na ni kampuni kwahiyo mimi kazi zangu zote zitakuwa zinauzwa kupitia kampuni hiyo. Nipo chini ya Wasafi.Com siyo WCB ingawa Wasafi.Com ndio Wasafi WCB. kwahiyo kazi zangu zote zitakuwa zinauzwa kupitia Wasafi.Com.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents