Burudani

Rayvanny awashukuru Basata kwa kuwapa ruhusa ya kufanya matamasha nje ya nchi

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva kutoka lebo ya muziki hapa nchini iliyopo chini y Diamond Platnumz, Rayvanny ametoa shukurani zake kwa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

Msanii huyo ametoa shukurani hizo baada ya kupewa ruhusa na Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) kwa kuwapa ruhusa yeye na boss wake Diamond Platnumz kufanya matamasha nje ya nchini baada ya kufungiwa kufanya matamsha kutokana na kukiuka baadhi ya masharti.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika haya:-

” NICHUKUE NAFASI HII KUSHUKURU BASATA, HUSUSANI BODI YA BASATA KWA KUTUPATIA RUHUSA YA KUFANYA MATAMASHA TULIOYAFANYA NCHINI #COMORO , #NAIROBI NA #MOMBASA .MATAMASHA TULITAKIWA TUSIYAFANYE KUTOKANA NA MAKOSA TULIYOYATENDA ILA KWA UPENDO WENU MLITURUHUSU KUYAFANYA. NITOE SHUKURANI ZANGU ZA DHATI KWENU MAANA BILA NYIE KUTUPA RUHUSA NI MENGI YANGETUKUTA VIJANA WENU…. LAKINI PAMOJA NA YOTE YALIOTOKEA KWETU NI KAMA DARASA LA KUJUA WAPI TULIPOTELEZA, ILI MBELENI LISIJIRUDIE KOSA KAMA TULILOLIFANYA. TUNA AHIDI KUA VIJANA BORA NA MFANO KWA JAMII HUSUSANI KATIKA MAADILI NAAMINI BASATA NA BODI YA BASATA MNATUPENDA VIJANA WENU NA MNATAMANI KUONA TUNAFIKA MBALI KATIKA SANAA, TUNAOMBA SANA HEKIMA ZENU KATIKA HILI VIJANA WENU TUENDELEE KUCHAPA KAZI KAMA ANAVYOSISITIZA MH. RAIS MAGUFULI …… BY RAYMOND SHABAN / RAYVANNY 🙏🙏🙏🙏🙏” 

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents