Burudani

Rayvanny: Fahyma hawezi kuchukia, ni baada ya video na Gigy kusambaa

Baada ya video yake yenye utata na video vixen Gigy Money kusambaa, msanii wa Bongo Flava Rayvanny amesema Baby Mama wake ‘Fahyma’ hawezi kuchukia.

Mshindi huyo wa tuzo ya BET 2017 akiwa chini ya label ya WCB, ameiambia Times Fm kuwa yeye na mpenzi wake hawachungani, hivyo jambo hilo alilichukulia kawaida.

“Hawezi kuchukia, halafu pia mimi sichungwi am live my life, president of own life, so nobody anaweza akaingilia akasema usifanye hiki, so Fahyma hana noma sometimes anaweza akafanya vitu vyake mimi simuingilii,” amesema Rayvanny.

Kuhusu ukaribu wake na Gigy Money, Rayvanny amesema, “It’s just a joke, Gigy ni mshikaji wangu na ni wa Mbeya pia, namjua before hajanza mbwembwe zake na ni mtu ambaye yupo happy muda wote mimi naona anaenjoy maisha yake”. Rayvanny na Fahyma amejawali mtoto mmoja wa kiume aitwae Jaydan.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents