Habari

RC Makonda amshukuru Mungu kwa kumpa maadui ‘bila wao ningeshindwa kuvuka bahari ya shamu’

Leo Februari 15 Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda anasherehekea siku yake ya kuzaliwa ambapo amemshuru Mungu kwa kumpa maadui kwani ndio waliomfanya kufikia hapo alipo.

RC Makonda ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika “Asante Mungu kwa kunipa mwaka mwingine tena , hii inaonyesha upendo na dalili njema ya bado nahitajika kufanya kusudi lako ndani ya dunia hii.Nakutukuza kwa ajili ya familia ,wazazi,ndugu na marafiki ambao wamekuwa nguzo na sehemu ya mafanikio yangu katika kukutumiakia wewe.”

Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar Es Salaam ameendelea kushukuru kwa kuandika “Asante pia kwa maadui ulio nipa kwani bila wao ningeshindwa kuvuka bahari ya sham“.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents