Michezo
Real Madrid na Atletico Madrid marufuku kusajili
Mahasimu soka wa Uhispania Real Madrid na Atletico Madrid wamepigwa marufuku kutonunua wachezaji wapya sokoni kwa vipindi viwili.
Klabu hizo mbili zimeadhibiwa na shirikisho la soka duniani Fifa baada ya kukiuka sheria za uhamisho wa wachezaji kuhusu kununuliwa kwa wachezaji ambao bado ni watoto.
Lakini marufuku hiyo haitaathiri kipindi cha sasa cha kununua wachezaji, ambacho kinaendelea hadi mwisho wa mwaka huu.
Atletico pia wametozwa faini franka 900,000 za Uswizi ambazo ni sawa na pauni 622,000 za Uingereza, nao Real wakatakiwa kulipa franka 360,000 (£249,000).