Real Madrid wampata mrithi wa Zinedine Zidane
Baada ya Zinedine Zidane kutangaza rasmi kujiuzulu kukinoa kikosi cha Real Madrid mapema mwezi uliopita, hatimaye klabu hiyo imemtangaza kocha atakayerithi mikoba yake.
Julen Lopetegui
Madrid wamemtangaza kocha wa Timu ya Taifa ya Uhispania, Julen Lopetegui kuwa ndiye atakayerithi mikoba ya Zidane baada ya michuano ya Kombe la Dunia kumalizika mwezi ujao. hii ni kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na klabu ya Real Madrid.
Official Announcement: Julen Lopetegui will be the #RealMadrid coach after the celebration of the 2018 World Cup.https://t.co/QcDiu6UjHV pic.twitter.com/iA1PnUdrtT
— Real Madrid C.F. π¬π§πΊπΈ (@realmadriden) June 12, 2018
Julen Lopetegui alishawahi kuzinoa klabu nyingi barani Ulaya ikiwemo FC Porto ya Ureno hii ni kabla ya kuingia kandarasi kuifundisha Hipania.