Michezo

Real Madrid wampata mrithi wa Zinedine Zidane

Baada ya Zinedine Zidane kutangaza rasmi kujiuzulu kukinoa kikosi cha Real Madrid mapema mwezi uliopita, hatimaye klabu hiyo imemtangaza kocha atakayerithi mikoba yake.

Julen Lopetegui

Madrid wamemtangaza kocha wa Timu ya Taifa ya Uhispania, Julen Lopetegui kuwa ndiye atakayerithi mikoba ya Zidane baada ya michuano ya Kombe la Dunia kumalizika mwezi ujao. hii ni kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na klabu ya Real Madrid.


Julen Lopetegui alishawahi kuzinoa klabu nyingi barani Ulaya ikiwemo FC Porto ya Ureno hii ni kabla ya kuingia kandarasi kuifundisha Hipania.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents