Habari
Red Ribbon show kufanyika Dec 23
Tanzania Mitindo House imeaanda onyesho la mavazi linalojulikana kama ‘Red Ribbon’ ikiwa ni kwa dhumuni la kuchangia kituo cha watoto yatima walioathirika kwa ugonjwa wa Ukimwi kilichopo chini ya Mitindo House.
Khadija Mwanamboka, mwenyekiti wa Tanzania Mitindo House aliongea na Bongo 5 kwa njia ya simu na kusema kuwa harambee hiyo itafanyika Desemba 23 mwaka huu katika hoteli ya Double Tree Hotel.
Mwanamboka aliongezea kwa kusema kuwa onyesho hilo la mavazi la Red Ribbon litaelekeza kuchangia gari kwa ajili ya kituo hicho cha watoto yatima, huku show hiyo ikisindikizwa burudani nyinginezo.