Burudani

Rick Ross ajutia kauli yake

Rapper kutoka Marekani, Rick Ross ameomba radhi kwa jamii juu ya kauli ya kutosaini wanawake kwenye lebo yake kwani angewasaini lazima angekuwa na mahusiano nao wa kimapenzi.

Rick Ross ameomba radhi kupitia kipindi cha redio cha ‘The Breakfast Club’. Boss huyo wa Maybach Music Group(MMG) ameamua kurudisha mdomoni matamshi yake aliyotoa siku ya jana na kukiri kosa hilo.

Ross amesisitiza  kuwaelimisha jamii yake kuacha kutoa matamshi mabaya dhidi ya wanawake. Pia anafikiria kutafuta rapper wa kike wanofanya vizuri na kuwasaini.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents