Michezo
Rihanna apanga kuinunua klabu ya Liverpool
Hivi karibuni kulikuwa na ripoti kuwa muimbaji wa ‘Diamond’ Rihanna ana mpango wa kununua klabu ya soka ya nchini Uingereza lakini haikufahamika ni ipi.
Na Jumanne hii gazeti la El Mundo Deportivo limethibitisha kuwa klabu hiyo ambayo Riri anataka kuinunua si nyingine bali ni Liverpool! Hiyo ni baada ya muimbaji huyo kupewa ushauri na mshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba wa klabu ipi anaweza kuinunua.
Liverpool inamilikiwa na kampuni ya Marekani, Fenway Sports Group.