Burudani
Rihanna atua Uingereza na bilionea wake
Mwanamuziki Rihanna ametua nchini Uingereza siku ya Jumatatu, kimya kimya na mwanaume anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake .
Mrembo huyo aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa nchi hiyo uitwao Heathrow, na kijana Hassan Jameel mwenye asili ya Saudia Arabia.
Hata hivyo Rihanna na Hassan walipishana muda mchache kuwasili uwanjani huo. Kumekuwa na tetesi hivi karibuni kuwa wawili hao wameveshana pete ya uchumba.