Habari

Rihanna kutoa album mbili kwa mpigo mwakani (2014)

Mwimbaji kutoka Barbados Robyn Rihanna Fenty maarufu kwa jina la jukwaani Rihanna, anaumaliza mwaka 2013 bila kutoa album yoyote. Album yake ya mwisho ‘Unapologetic’ ilitoka November 2012.

riri 4

Kuna tetesi kuwa mwimbaji huyo wa ‘Stay’ anatarajiwa kutoa album mbili kwa mpigo mwakani (2014).
Chanzo kimoja kimeliambia gazeti la ‘The Sun’ kuwa mpango wa RIRI ni kutoa album mbili kwa pamoja na Rihanna anatarajia kuwa na hits katika album zote mbili. “The plan is to put two records out. Rihanna wants big hits on both the albums.”

Baada ya kutoa ‘Unapologetic’ mwaka jana Riri amekuwa busy akinenepesha akaunti zake za benki kwa show za ‘Diamonds World Tour’ ambazo alianza kuzunguka March mwaka huu.

Mpaka sasa Rihanna ana album saba za studio na itakayofuata itakuwa ya nane.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents