Beki wa zamani wa timu ya taifa ya England na Manchester United, Rio Ferdinand jana alizawadiwa tuzo ya heshima kwa kuitumikia timu yake hiyo ya zamani ya Manchester United kwa miaka 12 kabla ya kuhamia QPR msimu huu.
Gwiji wa Manchester United, Sir Bobby Charlton ndiye alimkabidhi zawadi hiyo. Tukio hilo lilifanyika kabla ya mechi kuanza iliyokuwa ikichezwa kwenye uwanja Old Traford ambapo Rio alishangaliwa na kupigiwa makofi ya heshima.
Mechi hiyo iliisha kwa Man United kushinda mabao 4-0.