Burudani

Ripoti: Kanye West aomba ‘poo’ kwa Jay Z

Unatamani kuona urafiki wa Jay Z na Kanye West unarudi tena? Basi Kanye ameona bora yaishe.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, umeripoti kuwa Kanye ameomba kukutana na Jay uso kwa uso kwenye meza moja ili kuyamaliza matatizo yao.

Ugomvi wa wawili hao uliibuka zaidi baada ya Kanye West kuitaja familia ya Jay na mkewe Beyonce wanaitenga familia yake ikiwemo Blue Ivy kukatazwa kukutana kucheza pamoja na mtoto wao North West. Hata hivyo Jigga alijibu mapigo kupitia wimbo wake wa ‘Kill Jay Z’ ambao unapatikana katika albamu yake mpya, 4:44.

Inadaiwa kuwa mkutano huo wa kuzika bifu la Kanye na Jay litahudhuriwa na wakongwe wengine wa Hip Hop.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents