Burudani

Rita Ora: Nitawashukuru Jay Z na Beyonce daima

​Muimbaji wa Uingereza, Rita Ora aliyekuwa amesainishwa na label ya Jay Z, Roc Nation amesema bado rapper huyo na mkewe Beyonce ni watu muhimu kwake.

Alizungumza hayo kwenye mahojiano na jarida la September la Cosmopolitan.

Licha ya kupelekana mahakamani na  Roc Nation pamoja na tetesi za kuwa mchepuko wa Jay Z, Rita amedai kuwa hana bifu na Hov na Bey.

“Bado nina furaha nilikuwa na muda wa kuvutia. Jay ni mmoja wa idols wangu na Beyoncé ni wazi kuwa ni malkia wa maisha. Siwezi kuacha kushukuru mambo niliyopitia nikiwa nao na vitu nilivyoona.” 

Aliongeza kuwa mastaa hao ni walimu wazuri na anawatazama kama mfano.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents