Michezo
Roberto Di Matteo ateuliwa kuwa kocha mpya wa Schalke
Kocha wa zamani wa Chelsea, Roberto Di Matteo amepewa jukumu la kufundisha klabu ya Schalke 04.
Kocha huyo amepata kazi hiyo baada ya Jens Keller kutimuliwa Jumanne hii kama kocha wa klabu hiyo ya Ujerumani kutokana na mwanzo mbaya wa msimu.
Di Matteo alikuwa kocha wa Chelsea iliyoshinda ligi ya mabingwa Ulaya mwaka 2012, kwa kuifunga Bayern Munich katika uwanja wake wa Allianz Arena nchini Ujerumani. Alikuja kufukuzwa katika msimu uliofuata.