Burudani
Roberto wa Amarula kufanya kolabo na msanii wa Tanzania
Msanii wa Zambia anayehit na wimbo wake, Amarula, Roberto pamoja na msanii wa Tanzania Galaxy, wanatarajia kuingia studio kufanya kolabo.
Galaxy amesema tayari wameshafanya mazungumzo na msanii huyo na kinachofuata ni kuingia studio.
“Kolabo hatujaifanya bado kwa sababu kuna kazi fulani zilitokea. Kwahiyo tukawa tumepanga tufanye siku nyingine kwa sababu si unajua nilikutana naye kwenye show. Lakini kuanzia sasa kolabo itafanyika muda wowote kwa kuwa kila kitu kimeshawekwa tayari. Yeye atafanya vocal kwao na mimi nimeshafanya kila kitu.”