Michezo

Robin van Persie amuokoa kitanzini Moyes, ushindi dhidi ya Olympiakos waamsha matumaini ya mashetani wekundu

Hatimaye wachezaji wa Manchester United jana wamecheza tena kama vijana wa Fergie. Kwa mara ya kwanza tangu David Moyes aanze kukinoa kikosi hicho, United jana imecheza mchezo mkali zaidi na kuwapa ushindi dhidi ya Olympiakos uliowafanya waingie kwenye robo fainali ya ligi ya mabingwa wa Ulaya.

article-2584625-1C6E009500000578-790_634x437

article-2584625-1C6E286000000578-178_634x423
Fergie alikuwepo uwanjani kushuhudia vijana wake

Ni Robin van Persie ndiye aliyemuokoa kitanzini Moyes kwa kupunguza presha ya kutimuliwa iliyokuwa imemfikia shingoni baada ya kupachika mabao matatu ya nguvu na moja likiwa la mkwaju.

article-2584625-1C6E07DB00000578-753_306x423
Shujaa wa mchezo

Ushindi huo umewapa Manchester United walau pumzi ya kupumzika na kunywa maji kwa raha baada ya Jumapili iliyopita kutandikwa bao 3-0 na Liverpool kwenye ligi kuu ya England.

article-2584625-1C6DEAC800000578-699_634x421

Pamoja na van Persie kuwa shujaa wa mechi hiyo, Moyes anapaswa pia kumshukuru mlinda mlango wake, David De Gea ambaye aliokoa mipira hatari kutoka kwa David Fuster na Alejandro Dominguez muda mfupi kaba Van Persie kufunga goli la pili.

article-2584625-1C6DF98900000578-864_634x414
David De Gea akishangilia ushindi
article-2584625-1C6E39CD00000578-794_634x467

article-2584625-1C6E22A100000578-895_634x364
Pamoja na kufunga magoli matatu, Van Persie aliumia goti na kutolewa nje kwa machela
article-2584625-1C6E360200000578-37_634x434
Moyes, ambaye mustakabali wake ulikuwa matatani, alionekana na tabasamu pana usoni baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa

article-2584625-1C6DC21500000578-351_634x431
Valencia akisikiliza maumivu ya jicho baada ya kupigwa kichwa

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents