Michezo

Robson-Kanu wa Wales aingia kwenye 18 ya Lionel Messi

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Wales na klabu ya West Bromwich Albion ya Uingereza, Robson-Kanu amefanikiwa kuingia kwenye vita ya kuwania tuzo ya goli bora kwa mwaka 2016 maarufu kama Puskas Awards akiungana na wachezaji wengine 10 akiwemo Lionel Messi.

js92322551

Robson-Kanu amefanikiwa kuingia kwenye orodha hiyo kutokana na goli alilolifunga kwenye robo fainali ya kombe la Euro dhidi ya Ubelgiji mwezi Juni mwaka huu.

Wachezaji wengine waliotangazwa kuwania tuzo hiyo ni: Mario Gaspar (Spain), Hlompho Kekana (South Africa), Marlone (Brazil), Lionel Messi (Argentina), Neymar (Brazil), Saul Niguez (Spain), Daniuska Rodriguez (Venezuela), Simon Skrabb (Finland) na Mohd Faiz Subri (Malaysia).

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents