Burudani

Roma awaonya wanasiasa

 

Rapper katika Game ya Bongo flava Roma Mkatoliki, amevishukia vyama vya Upinzani vinavyotumia ngoma zake za Pastor na Tanzania katika kampeni zao za kisiasa bila ruhusa yake.

Roma amesema amewahi kushuhudia moja wapo ya Kampeni ya kisiasa ikitumia nyimbo zake na amevionya vyama hivyo kuacha mara moja, au wamfuate kuongea nae ili waelewane kibiashara.

Roma amesema ametoa muda kwa Vyama vya siasa vya Upinzani vinavyotumia ngoma zake katika mikutano yao na kampeni kumfuta ama kuacha kutumia, la sivyo atachukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika hao, kwani wao wananufaika kwa kuwavuta mashabiki kwa kivuli cha nyimbo zake.

Sikiliza ngoma yake ya ‘Mr President’ hapa.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents