Burudani

Roma Mkatoliki apigwa ‘STOP’ kufanya muziki, Nay wa Mitego apewa onyo kali (+video)

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Sanaa na Utamaduni imemfungia kifungo cha miezi sita msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Roma Mkatoliki kutojihusisha na shughuli zozote za muziki baada ya kukaidi agizo la kubadilisha wimbo wake wa Kibamia.

Roma Mkatoliki

Akitoa adhabu hiyo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza amesema kuwa Roma amedharau wito wa serikali ambapo leo aliitwa ili ahojiwe  kutokana na wimbo wake huo ikiwa ni hatua ya pili mara baada ya Baraza la Sanaa Nchini Basata kumuita na kumtaka arekebishe baadhi ya sehemu katika wimbo huo.

Mhe. Shonza amesema kuwa adhabu hiyo itajumuisha na nyimbo zake zote kutokupigwa Redioni wala kwenye runinga kwa muda wote aliyofungiwa.

Soma na Hii – Roma Mkatoliki adai BASATA wameshindwa kumpa majibu

Kwa upande mwingine, Mhe. Shonza amesema Serikali itaangalia mwenendo wa msanii wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego ambaye naye aliitwa na kukiri makosa na kuahidi kubadilika.

Tazama video hapa chini;

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents