MichezoUncategorized

Romelu Lukaku aamua kuingia kwenye muziki (+Video)

Romelu Lukaku aamua kuingia kwenye muziki (+Video)

Mchezaji wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Ubelgiji, Romelu Lukaku ameamua kujiingiza kwenye muziki mbali na kuchezaji mpira.

Mchezaji huyo ameamua kujiingiza kwenye muziki baada ya kuomba kufanaya kolabo na rapper kutoka Ubelgiji anayejulukana kwa jina la The Color Grey.

Akiandika kwenye ukurasa wake wa Instagram Rapper huyo amesema:- ” A while ago the homie @romelulukaku asked me to make a track together that pays homage to his childhood and rise to where he is today. I didn’t have to think twice since we share the same background and carry that same hunger!”

“Kuna kipindi ndugu yangu Romelu lukaku aliniomba kufanya nyimbo pamoja na mimi ambao alitaka kuelezea maisha yake tangu utotoni hadi hapa alipofikia katika maisha yake na kusaidia kuinuka vipaji kutoka Ubelgiji. Baada ya kuniomba hili Sikuwa na muda wa kufikiri mara mbili kwa tulishirikiana tangu utotoni kwani historia zetu zinafanana pia tulishirikiana uwanja mmoja,tulilala na njaa wote!”


Ikumbukwe kwamba Lukaku pamoja na mchezaji mwingine wa Manchester na raia wa Ivory Cost Eric Baily wako chini ya kampuni ya mwanamuziki kutoka Marekani Jay Z inayohusika kwenye mambo ya usaji ikiwa kama Agent wa wachezji hao inayojulikana kwa jina la Roc Nation Sports.

Lukaku hajaonekana uwanjani kwa takribani wiki sasa kutokana na majeraha yake ambayo yamemkosesha baadhi ya michezo ikiwemo katika timu yake ya taifa ambayo kwa sasa wanacheza michuano ua UEFA Nation League na katika mchezo wa jana usiku walipoteza kwa jumla ya goli 5-2 dhidi ya Uswisi.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents