Michezo
Ronaldo akutwa na Virusi vya Corona
Cristiano Ronaldo amekutwa na virusi vya Corona na sasa ataukosa mchezo wa siku ya Jumatano ambapo Ureno itawakabili Sweden.
Ronaldo akutwa na Virusi vya Corona
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 35, tayari ameshajitenga ili kuepusha kuusambaza ugonjwa huo kwa mtu wingine.
Taarifa zimekuja mara baada ya mshindi huyo mara tano ya tuzo ya Ballon d’Or akiwa ameshacheza mchezo dhidi ya Ufaransa katika michuano ya Nations League na mechi ya kirafiki na Hispania.
Kabla ya taarifa hizo za Corona kutolewa, Ronaldo alishakuwa pamoja na baadhi ya wachezaji wengine kwa kusalimiana na hata kupata picha ya pamoja.