Michezo

Ronaldo amuonya Philippe Coutinho kujiunga Barcelona

Aliyekuwa mshambuliaji hatari wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vikubwa vya Ulaya, Ronaldo Luís Nazário de Lima amemuonya kiungo wa Liverpool, Philippe Coutinho kuhusu kujiunga na Barcelona.

Coutinho ambaye amekuwa akiwindwa na vinara hao wa La Liga tangu msimu uliopita, ameambiwa na Ronaldo kuwa Barca ni timu ambayo imekuwa na matatizo makubwa na wachezaji wa kutoka nchini Brazil.

Nilijisikia furaha zaidi na zaidi nilipojiunga na Real Madrid, licha ya kuwa nilikuwa na mwaka mzuri huko Barcelona,” Ronaldo amesema hayo wakati akiongea na kituo cha runinga cha Esporte Interativo.


Ronaldo de Lima akiongea na kituo cha runinga cha Esporte Interativo

“Mwishoni, historia yangu na Barça ilikuwa mbaya sana, sawa na ile Neymar aliyokuwa nayo. Barcelona daima imekuwa na matatizo na wachezaji wa Brazil: Neymar, Romario, Ronaldinho na mimi. Sisi wote tulitendewa vibaya na klabu mwishoni licha ya michango yetu yote na kujitolea,” ameongeza.

De Lima aliichezea Barca kwa msimu mmoja wa mwaka 1996–1997 katika mechi 37 na alifanikiwa kufunga magoli 34 na baadaye alihamia Inter Milan ambapo alicheza kwa misimu mitano.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents