Ronaldo kurejea uwanjani kuikabili Udinese, kocha wa Juventus amwagia sifa
Mshambuliaji hatari duniani anaekipiga ndani ya klabu ya Juventus, Cristiano Ronaldo anatarajiwa kurejea uwanjani hapo kesho kuikabili timu ya Udinese.
Nyota huyo hatari kunako mchezo wa soka anakabiliwa na tuhuma za kumbaka mwanadada, Kathryn Mayorga raia wa Marekani ambaye amesema kuwa kitendo hicho amefanyiwa mwaka 2009 huko Las Vegas.
🎙 @OfficialAllegri: "Tomorrow I could go with a front three of @MarioMandzukic9, @PauDybala_JR and @Cristiano, or one of them could be rested. @Cuadrado is in good form and his assist the other night has provided a boost."#UdineseJuve
— JuventusFC 🇬🇧🇺🇸 (@juventusfcen) October 5, 2018
Licha ya timu ya taifa ya Ureno kutangaza hapo jana kuwa haitamjumuisha Ronaldo ndani ya kikosi hicho, mchana huu meneja wa klabu ya Juve, Massimiliano Allegri amethibitisha kuwepo kwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 hapo kesho.
“Namfahamu Cristiano kwa miezi mitatu sasa na kwazaidi ya miaka 15 katika fani yake amekuwa akionyesha taaluma bora ndani na nje ya uwanja. Yupo tayari kwa kurejea hapo kesho,” amesema Allegri.
🎙 @OfficialAllegri: "I've known @Cristiano for three months now and for over 15 years of his career he has shown to be a great professional both on and off the pitch. He is ready to return to action tomorrow."#UdineseJuve pic.twitter.com/tOJt6Lq7g6
— JuventusFC 🇬🇧🇺🇸 (@juventusfcen) October 5, 2018
Siku ya Jumanne Ronaldo alikuwa nje ya uwanja akishuhudia timu yake ya Juve ikiibuka na ushindi wa jumla ya mabao 3 – 0 dhidi ya Young Boys michuano ya Champions League baada ya kupewa adhabu ya kutocheza mechi moja kutokana na kumtendea mazambi mchezaji wa Valencia.
SIIIIIIIII!!!!! 🔥 @Cristiano finds the target! ⚽
🖥 Watch the full video on https://t.co/8iZ5bhkzPZ ⏯ https://t.co/XAN4kVjZ0z #ForzaJuve #CR7JUVE pic.twitter.com/fUkJaY6HuH
— JuventusFC 🇬🇧🇺🇸 (@juventusfcen) October 4, 2018