Rose Ndauka asilimu dini kisa Love la Mbongo fleva
kama H.Baba. Hawa wanaweza kuwa mifano mizuri kati ya wasanii wengi ambao wanachanganya, hasa katika kusaka mshiko ili kula sahani moja na hali harisi ya maisha.
Bado hawakuishia katika kuingiliana katika kazi za kisanii ila wameamua kufika mbali zaidi katika maisha, huenda wapo wanafanya kweli na wapo wamegeuza kama fasheni yaani msanii wa filamu kuwa na uhusiano na msanii wa muziki.
Hivi juzi mwanamuziki Rose Ndauka, ametangawa wazi kwamba anauhusiano wa kweli na unaojulikana hadi kwa wazizi na mwanamuziki Maliki Bandawe. Hapa tunasema ameungana na mwigizaji mwenzake wema katika kutangaza wazi kwamba amezama in Love na waimbaji wa Bongo Fleva Diamond.
Wema yeye alikubali kuvishwa pete, huku tukisikia stori za wengine kama mwigizaji Jack wa Chuzi na mbongo fleva Timburo na hata marachache tulisikia ya mbongo fleva Barnaba na na mwigizaji Shilole.
Huu ni wakati wa Rose Ndauka, ambaye kwa sasa ameshabadili jina na kuitwa Aisha, Kama ilivyokuwa kwa Witnes kubadili dini kwaajili ya Monkeyz.
Ila Rose Ndauka amesema yeye amebadili dini kwaajili mama yake kuwa muislam, lakini pia kwa upande mwingine ni msukumo wa kijana toka Tanga… yaani Tanga yalikozaliwa mapenzi Maliki.
Hivi sasa Rose amesema anapenda kuitwa Aisha ingawa kwenye tasnia ya filamu atajulikana kama Rose Ndauka. Na ukitaka kumjua bwana wake hebu muangalia katika wimbo wa Bongo. Com ya TNG Squad kikundi kilichokuja kwa kasi kikalewa na umaarufu kikavunjika(Jamaa aliyevaa kofia mwenye sauti nzito upande wa Chorus).
Hongera Rose Ndauka kwakuwa umesikika ukisema kwamba hutobadilika tabia, na hutishiki na kauli ya ndoa za mastaa hazidumu.
By Moe One’s
{hwdvs-player}id=1686|width=560|height=340{/hwdvs-player}