Michezo
Saa 48 zatosha kwa Arsenal kuingia kandarasi na kiungo huyu hatari wa Uruguay
Kiungo wa Sampdoria, Lucas Torreira yupo njiani kuelekea jijini London kwaajili ya kwenda kukamilisha vipimo vya afya ili kukamilisha dili la kutua Arsenal saa 48 kuanzia sasa.
Kiungo wa Sampdoria, Lucas Torreira
Inafahamika kuwa gharama za mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Uruguay ni pauni milioni 26 bila ya kiasi cha fedha binafsi huku ikionekana hilo si tatizo kwa Arsenal.
Matteo Guendouzi
Arsenal pia ipotayari kutoa gharama za pauni milioni 8 kwa klabu ya Lorient kwaajili ya Matteo Guendouzi ambaye ambaye amekuwa akihusishwa pia kuhitajika timu za Tottenham pamoja na Manchester City.
Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya vijana nchini Ufaransa anatarajiwa pia kufanyiwa vipimo vya afya wii hii ili kukamilisha dili hilo.