Habari
Sad News: Baby Madaha amefiwa na Mama yake mzazi
Tumepokea kwa huzuni kubwa taarifa za Baby Madaha kufiwa na mama yake mzazi jana usiku ambaye amekuwa akiumwa ka muda, habari zilizotufikia ni kwamba mwili wa marehemu unasafirishwa kupelekwa Musoma nyumbani kwao ambapo mipango yote na taratibu za kuzika zitajulikana.
“Naumia sana lakini najua yote ni mipango ya Mungu kwani kila kitu kimepangwa, hivyo tunamuombea mama yetu aweze kwenda salama mbele za haki kwani sote hiyo ndiyo njia yetu” alisema Baby Madaha.
Bongo5 tunawaombea Mungu awaongoze katika wakati huu mgumu kwenu, hakuna kama mama. May her soul rest in eternal Peace.