Burudani

Safari ya Ben Pol Ufaransa yazaa matunda

Msanii wa muziki wa R&B, Ben Pol amefunguka kwa kudai kwamba tayari amefanya kolabo na wasanii kadhaa kutoka nchini Ufaransa.

Muimbaji huyo alikuwa nchini humo wiki kadhaa zilizopita kwa mualiko maalum baada ya kuchaguliwa kuwa balozi na taasisi moja ya kusaidia watoto ya nchini humo.

Akiongeza na Bongo5 wiki hii, Muimbaji huyo ambaye anajipanga kuachia wimbo wa kufunga nao mwaka, amedai safari ya ufaransa aliitumia vizuri kwaajili ya muziki wake.

“Mungu ni mwema kuna kazi kadhaa nilibahatika kufanya lakini kwa sasa ni mapema zaidi kuzizungumzia,” alisema Ben Pol.

Aliongeza, “Muziki umekuwa na ushindani mkubwa hivyo ukipata nafasi lazima uitumie ipasavyo. Kwahiyo wakati nipo kule nilipata nafasi ya kukutana baadhi ya wadau na kufanikiwa kutengeneza baadhi ya kazi ambazo kwa sasa ni mapema zaidi kuzizungumzia,”

Muimbaji huyo alikuwa ni mmoja kati ya wasanii waliofanya vizuri weekend iliyopita katika tamasha kubwa la fiesta.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents