Safari Ya Kocha Wa Stoke City
David Seamen akiwa na waongoza watalii wa kampuni ya Zara Adventure mlima Kilimanjaro walikopanda Mei 19 kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kituo cha watoto cha Donna Luis Hospice cha nchi Uingereza.
Kocha Tony Pulis akimkabidhi mpira mwandishi wahabari wa Globu ya Jamii na mkoa wa Kilimanjaro Dixon Busagaga baada ya kuutia saini.
Tony Pulis akitoa zawadi ya kikombe kwa nahodha wa timu ya Zara Tours, John. Zara Tours ndio mabingwa wa mashindano ya kampuni za utalii mkoa wa Kilimanjaro.
David Seamen akionyesha ishara ya ushindi mara baada ya kurejea salama kutoka mlima Kilimanjaro alikopanda na wenzake 13.
Kocha Pulis akionyesha jezi ya timu ya Zara Tours iliyosainiwa na wachezaji wa timu hiyo aliyopewa kama kumbukumbu ya kuja nchini kupanda mlima.