Michezo

Safari ya Mourinho ndani ya Manchester United kufikia tamati mwezi wa tisa

Taarifa za andani ya klabu ya Manchester United zinaeleza kuwa wachezaji wa timu hiyo pamoja na wafanyakazi wanaamini meneja wao Jose Mourinho huwenda akatimuliwa kazi endapo atapoteza katika mchezo wao wa Jumapili ya terehe 01/09/ 2018 dhidi ya Burnley.
Kiongozi wa United, Ed Woodward amefanya mazungumzo na Mourinho juma hili kufuatia timu yao kupata matokeo mabaya mfululizo dhidi ya Brighton na Tottenham.

Wachambuzi wa mambo wanaamini kikao hicho kinafanana na kile alichofanyiwa meneja, Louis van Gaal katika siku zake za mwisho mwaka 2016 na nafasi yake kuchukuliwa na Mourinho ambaye kwa sasa kunauwezekano mkubwa wa Zinedine Zidane kurithi mikoba hiyo.

Chanzo hicho kutoka ndani ya Manchester United kimesema kuwa ”Muda si mrefu, Jose atatimuliwa wengine wakiamini ataondoka endapo atapoteza mbele ya Burnley na wengine wakiamini hatokuwepo mwanzoni mwa mwezi wa tisa ,” kimesema chanzo hicho.

Inaelezwa kuwa wachezaji nane pekee ndiyo waliyoungana meneja wao, Mourinho kutoka kwenye viunga vya Carrington kwenda kwenye hoteli yao ya the Lowry baada ya kumalizika kwa mechi yao na Spurs wakati wengine wakiamua kuondoka binafsi huku Paul Pogba akitumia gari lake.

Related Articles

3 Comments

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents