Burudani

Said Fela amkabidhi Temba nyumba yake ya pili

Said Fela amemkabidhi Mheshimiwa Temba nyumba yake ya pili. Rapper huyo wa TMK Family, amesema kuwa nyumba aliyokabidhiwa na Fela imepatikana kutokana na mauzo ya kazi zake za muziki ndani ya TMK Family.

k
Picha aliyoposti Mkubwa Fela na kuandika ujumbe huo

Temba amesema kuwa utaratibu huo ulikuwepo toka zamani ambapo kila msanii kutokana na fedha alizoingiza kupitia kazi zake hununuliwa kiwanja au kujengewa nyumba.

“Huo ni utaratibu ambao tulikuwa nao toka zamani,”Temba aliiambia Bongo5. “Wakati wapo akina Nature na wasanii wote wa TMK kwamba Mkubwa Fela alikuwa anatusimamia anatuahidi mauzo yatokayouzwa kwenye album alisema atanunua kiwanja na ujenge nyumba,kwahiyo nyumba nimeshajenga lakini kwa usimamizi wake yeye kwa kutumia kazi zangu.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents