Burudani
Said Fella kujitosa kwenye biashara ya album za muziki
Dully Sykes anatarajia kutoa album yake ambapo amekubaliana na meneja wa Mkubwa na Wanawe, Said Fella kumuuzia master album itakayokuwa na nyimbo zake za zamani pamoja na nyimbo chache mpya.
Akiongea na 255 ya XXL (Clouds FM), Fella alisema ameamua kuongea na wasambazaji ili wafanye biashara ya album kwa sababu kuna watu wananunua nakala sizizo halali na kwamba mpango huo utaanza mwezi wa tano.
Alisema ataanza na album ya Yamoto Band na kisha album ya Chege na Temba, Berry Black, THT, Barnaba, Shaa na Diamond Platnumz.
Jumla kutakuwepo na album 10.