Burudani
Saif al-Adel mrith wa Osama bin Laden
Kundi la Al- qaida limepata kiongozi mpya Saif Al-Adel ambaye amekuwa akiongoza katika mashambulizi mbali mbali ambayo yameikumba dunia kipindi kilichopita na kuwa mtu muhimu sana mbele ya kiongozi wa kundi hilo ambaye ameaga dunia hivi karibuni Osama Bin Laden.
Jina ambalo anatamba nalo ni Upanga wa Sheria, ameshahusishwa na matukio mengi yakiwemo ya kupanga mashambulizi katika ubalozi wa Marekani Tanzania na Kenya mwaka 1998. Ingawa ni raia wa Misri lakini pia inasemekana alipanga mashambulizi ya kumuua raisi wa nchi hiyo Anwar Sadat 1981.
Pia amekuwa akitoa mafunzo kwa wanaharakati mbalimbali wa kijahidina, na waipslamu ambao wamekuwa wakitetea haki zao katika nchi mbambali ikiwemo Parestina.