Saini ya Mbwana Samatta yawa lulu kwa klabu hizi tatu za Uingereza!
Huwenda msimu ujao mtanzania Mbwana Samatta ambaye anakipiga katika klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji tukamshuhudia akisakata kabumbu katika ligi maarufu duniani ya EPL.
Mshambuliaji huyo amekuwa na msimu mzuri zaidi mwaka huu katika ligi ya Ubelgiji baada ya kufunga magoli 14 katika mechi 16.
Mtandao wa HITC umeripoti kwamba mchezaji huyo ambaye pia anafanya vizuri katika ligi ya Europa saini yake inawindwa na klabu za Uingereza kama West Ham United, Everton pamoja na Burnley .
Kwa mujibu wa mtandao wa Read Everton umeonyesha kumkubali zaidi mshambuliji huyo wa zamani wa TP Mazembe na Simba SC baada ya kuweka chati ya kupiga kura kama mchezaji huyo anaweza kusajiliwa na klabu hiyo kongwe Uingereza.
Mbwana Samatta hits a second-minute Genk opener against Lokomotiva Zagreb. Belgian side lead 3-2 on aggregate. #UEL pic.twitter.com/0OPA2qopNk
— UEFA Europa League (@EuropaLeague) August 25, 2016
Katika chati hiyo mashabiki wangi wameonekana kuamini kwamba mchezaji huyo anaweza kusajiliwa na Everton baada ya kupiga kura za ndio kwa 68% huku za hapana zikiwa 32%.
Hii huwenda ikiwa ishara nzuri kwa soka la Tanzania kwani Samatta amekuwa ni mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kufanya vizuri zaidi Ulaya.