Michezo

Sakata la kodi kwa wanasoka wageni nchini Uhispania laendelea kuwatafuna,Sasa ni zamu ya beki huyu wa Madrid kufikishwa Mahakamani

Sakata la kodi kwa wanasoka wageni nchini Uhispania laendelea kuwatafuna,Sasa ni zamu ya beki huyu wa Madrid kufikishwa Mahakamani

Imekuwa kama mazoea sasa kusikia mwanasoka wa kigeni anayeitumikia ligi ya Uhispania alimaarufu La liga  kuendelea kukumbwa na suala la ukimbia kodi.

Tulianza kuiona kwa baadhi ya wachezaji wakubwa waliowahi kuchezea ligi hiyo mfano mshambuliaji wa klabu ya Juventus Cristiano Ronaldo alikubwa na sakata la kukimbia kodi pia ikamkuta mchezaji mwingine anayeitumikia klabu ya FC Barcelona Lionel Messi ambapo alikumbwa na sakata kama hilo la kukimbia kodi lakini pia kocha wa Manchester United Jose Mourinho naye pia ilisemekana amekimbia kodi.

Baada ya hao wote kukumbwa na sakata hilo msiba umehamia kwa beki wa klabu ya Real Madrid na taifa la Brazil  Marcelo amekubali kulipa kiasi cha euro 75000 sawa na bilioni mbili za Kitanzania ikiwa kama faini ya ukwepaji kodi.

Marcelo atatokea mahakamani siku ya Jumanne kuomba mashtaka kuepuka kupelekwa jela baada ya mashtaka hayo ya kukwepa kodi pia ikiwa ni kupunguza faini. MBrazil huyo alihukumiwa kwa kosa la kuepuka malipo ya € 1m baada ya madai ya kuhamishwa picha yake katika kampuni ya Uruguay inayoitwa Birsen Trade SA ambayo alitumia kuzuia malipo ya kodi kwa hazina ya Hispania.

Mchezaji wa zamani wa Fluminense alikubali kutoa mambo yake kwa kampuni ambayo “haina rasilimali za kibinadamu na vifaa vya kutekeleza majukumu yake”, na mamlaka ilitawala kwamba alikuwa amekwisha kodi ya thamani ya takribani € 500,000.

Shirika la kodi pia linamshtaki Marcelo ya kuepuka malipo ya € 100,476 na € 101,615 kwa miaka ya 2011 na 2012.

 

By Ally Juma

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents