Salama Jabir na utani wa Kiswahili kwa Kanye West! Very funny!!
Kama Kanye West angekuwa anaelewa Kiswahili huenda angefanya kila awezalo ili aonane na mtangazaji wa kipindi cha Mkasi, Salama Jabir. Huenda pia Kanye ni miongoni mwa wasanii wa Marekani wanaomvutia Salama na kama angekuwa karibu angemtafuta kwa show ya Mkasi. Tunajiuliza angemuuliza maswali gani!! Maswali ya haraka haraka ambayo tunadhani Salama angemuuliza Kanye ni kwa mfano ‘Ni kweli uliangalia sex tape ya Kim na Ray J’!!
So hivi karibuni kupitia Twitter Salama amekuwa akimwandikia Kanye (kwa utani) mambo kibao kwa Kiswahili na kama ukisoma anayomwambia huenda ukakaribisha tabasamu usoni mwako ama kicheko kirefu. Bahati mbaya hajawahi kujibu.
Hizi ni baadhi ya tweets alizomwandikia Kanyewest:
Umesahau Kufunga Zipu Blaza…Ya Begi Lakooo… @kanyewest
Oooooi… Umelala Mdomo Wazi… @kanyewest
@kanyewest Unaweza fanya mpango ukatusapraizi na mvua huku?!
Kesho Ntakuambia Maana Ya Jina Lako Kwa Lugha Yangu… @kanyewest
Mshipi Wako Umevua Kitu?! Kitoweo Cha Familia Baba..Mama’ako Angekua Proud…Saaaana!! Amlaze Pema Jalali. @kanyewest
Unaangaliaga Pilau?! @kanyewest
Ushawahi kula kipilaaa?! @kanyewest
Bi Kidude Akikuuuona Tu Atakuambia “Mume Wangu Ulikua Waaapi?!” @kanyewest
Bi Kidude?! Kama Humjui Huyu Utakua Umefeli…Maana Unahitaji Kolabo Kwasababu Za Kibiashara… @kanyewest
Wakati Wa OPP Nlikua Kwetu Tanga…Nasoma Bombo Praimari…Wewe Je?! @kanyewest
Unaangalia Mechi?! @kanyewest Au Ushauza?!
Mwanangu Nna Mwanangu Kaaaaaama Weeeeewe… Kosa La Marehemu Baba! @kanyewest