Michezo
Samatta aifungia timu yake KRC Genk katika ushindi wa goli 4-1
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta anayeichezea klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji March 13 alipata nafasi ya kuanza katika kikosi cha Genk.
Alifanikiwa kufunga goli lake la kwanza akicheza katika kikosi cha first eleven na goli lake la pili toka ajiunge na klabu hiyo, Genk iliifunga Oostende kwa magoli 4-1 kwenye ligi ya Belgium Pro Leaue.
Magoli ya KRC Genk yalifungwa na Mbwana Samatta dakika ya 25, Balley dakika ya 39, Pozuelo dakika ya 81 na Camargo dakika ya 88, wakati goli la kufutia machozi kwa KV Oostende lilifungwa na Siani dakika ya 90.