Samatta aisaidia timu yake ya Genk kutwaa ubingwa wa Ubelgiji, awa kinara wa ufungaji, wachezaji wenzake wamuimbia nyimbo hii (+ Video)
Samatta aisaidia timu yake ya Genk kutwaa ubingwa wa Ubelgiji, awa kinara wa ufungaji, wachezaji wenzake wamuimbia nyimbo hii (+ Video)
Mshambuliaji wa Taifa StarsĀ na Klabu ya Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta ameisaidia klabu yake ya Genk kutwaa ubingwa wa Ubelgiji. katika mchezo wa mwisho baada ya sare ya 1-1 ya KRC Genk dhidi ya Anderlecht na kipigo cha Club Brugge cha 2-0 kutoka Standard de Liege KRC Genk wanatangazwa kuwa Mabingwa wa Ligi Kuu Ubelgiji 2018/2019 wakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Msimamo wa ligi uko hivi:-
Hawa ndio wafungaji bora wa ligi hiyo Samatta akiwa kinara wa ufungaji:-
Ubingwa huo umewapa KRC Genk nafasi ya kucheza UEFA Champions League hatua ya Makundi moja kwa moja msimu wa 2019/2020. Baada ya ushindi huo Wachezaji wenzake wa wa KRC Genk wakiwa dressing room baada ya kutangazwa Mabingwa wa Jupiler Pro League 2018/2019.
Baada ya kutangazwa Mabingwa KRC Genk walitembea katika bus la wazi na bus hilo likiwa na wachezaji na benchi la ufundi na baada ya kumaliza Party ilifanyika Limburghal saa 22:00 shabiki wa kawaida walilipia Euro 10 (Tsh 25,695).
Na wakati wa sherehe hizo Shabiki mmoja akiwa na bendera ya Tanzania katikati ya mashabiki wa Genk wakishangilia ubingwa.
By Ally Juma.