Michezo

Samatta huyu hatari, atupia UEFA Europa League kama kawaida

Mshambuliaji hatari wa klabu ya KRC Genk, Mbwana Samatta ameiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa jumla ya mabao 2 – 0 dhidi ya Malmo FF michuano ya UEFA Europa League.

Image result for KRC Genk vs Malmo Off 2 - 0

Katika mchezo huo uliyopigwa kwenye uwanja wa Luminus Arena, Samatta ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania ameipachikia bao la pili Genk kunako dakika ya 71 wakati la kwanza likifungwa Leandro Trossard dakika ya 37 ya kipindi cha kwanza.

Mchezaji huyo hatari ndani ya Genk anayewindwa na klabu kubwa barani Ulaya amekuwa na mwanzo mzuri katika kupachika mabao toka alipotoka kuuguza majeraha yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents