‘Sanaa sio uhuni’ – Snura
Msanii wa Bongo Fleva, Snura ameamua kuwachana watu wanaodai kuwa Sanaa imejaa uhuni kwa kuwazibua masikio kuwa uhuni ni tabia ya mtu na wala hauletwi na Sanaa.
Snura amesema Sanaa haileti uhuni hata siku moja kwani wapo watu ambao wanafanya uhuni na bado hawapo kwenye sanaa.
“Sanaa ni kazi kama kazi nyingine, haihusiani kabisa na uhuni kwani uhuni ni tabia tuu ya mtu mwenyewe nawashauri akina Mama wanaowakataza watoto wao kuingia kwenye sanaa wasiwakataze“Amesema Snura kwenye mahojiano yake na East Africa Radio.
Mkali huyo wa Chura ameenda mbali zaidi kwa kutoa mfano kuwa wapo akina Mama ntilie ambao hawapo kabisa kwenye sanaa na bado wanafanya uhuni.
“Ukisema Sanaa ni uhuni nakushangaa sana kwani wapo akina Mama Ntilie mtaani ni wahuni sana na hawapo kwenye sanaa“,Amesema Snura.