Habari
Sauti za Busara zafana
Sauti za Busara 2011 lilikuwa tukio lililofana zaidi ya mategemeo ya mashabiki na wadau wa muziki waliohudhuria. B5 inakuletea habari katika picha.
Mtoto wa Maureen Lupo Lilanda, akiwa stejini sambamba na mama yake, jambo ambalo lilipendeza mashabiki. Ilionyesha jinsi gani muziki ulivo tamaduni yao.
Waimbaji toka Mozambique, (Msumbiji) wakitoa burudani iliyofana sana
Muthon The Drummer Queen toka Kenya,akiwajibika. Aliweza kurapu katika miondoko ya kipee, kupiga ngoma za asili, huku akicheza. Aliwavuta mashabiki wa rika zote, na wa mataifa yote kutokana na staili yake ya upigaji uchezaji na uimbaji.
Lelele kutoka Kenya naye alionyesha uwezo wake wa kuimba taarab asilia, akisindikizwa na wapigaji nguli.