Habari

Sayansi ya ufufuaji: Miaka 20 ijayo madaktari watakuwa na uwezo wa kuwarudishia uhai wagonjwa waliokata roho!!!

Twende taratibu, hii ni taarifa ya kisayansi na sio ‘kiimani’ na imetolewa na daktari bingwa wa moyo wa Marekani. Sasa naomba uniruhusu nikuelezee nilichokutana nacho kuhusiana na habari hii.

dr

Dr Sam Parnia wa Marekani amedai kwamba kwa kupitia mbinu za kisasa za kitaalamu (kisayansi) kuna uwezekano wa kumrudishia uhai mgonjwa aliyekata roho ndani ya saa 24!! (hata mimi nimeguna)

Dr huyo wa moyo ambaye amepata mafunzo yake nchini Uingereza, ameendelea kusema hivi karibuni wanategemea kuanza kuokoa maisha ya wagonjwa wanaokuwa tayari wamekata roho katika masaa ya mwanzo baada ya kuthibitisha wamefariki. “We may soon be rescuing people from death’s clutches hours, or even longer, after they have actually died.” Alisema Dr Sam

Parnia ameendelea kutetea kauli hiyo kwa kusema kuwa muigizaji wa Marekani James Gandolfini aliyefariki mwezi uliopita angeweza kupona endapo angekuwa ameugulia tatizo lake la moyo New York.

“I believe if he died here, he could still be alive. We’d cool him down, pump oxygen to the tissues, which prevents them from dying, Clinically dead, he could then be cared for by the cardiologist. He would make an angiogram, find the clot, take it out, put in a stent and we would restart the heart,” Dr Parnia alilieleza jarida la Der Spiegel la Ujerumani.

dr-3

Dr Parnia ambaye ni mkuu wa kitengo cha ‘Intensive care’ katika hospitali ya the Stony Brook University iliyoko New York, Marekani aliendelea kusema ni kweli hawawezi kuokoa maisha ya kila mtu sababu wagonjwa wengi wa moyo huwa na matatizo mengine ya ziada na makubwa zaidi.

Aliendelea kusema kama teknolojia ya kisasa ya tiba na mafunzo vingekuwa vinafanyiwa kazi inavyotakiwa, (kitu ambacho anadai bado hakijafanyika) basi watu ambao wangetakiwa kufa ni wale tu wenye matatizo ambayo hayatibiki kabisa lakini sio ugonjwa wa moyo unaotibika.

’‘A heart attack is treatable. Blood loss as well. A terminal cancer isn’t, neither are many infections with multiresistant pathogens. In these cases, even if we’d restart the heart, it would stop again and again”.

Akielezea jinsi ambavyo mgonjwa wa moyo aliyefariki anavyoweza kurudishiwa uhai, alisema kwanza ni kuugandisha mwili mara tu baada ya kuthibitishwa amefariki , “freezing the body immediately after death – but cooling it down to best preserve brain cells while keeping up the level of oxygen in the blood. This buys time to fix the underlying problem and restart the heart”. Alisema

Dr huyo alisema kuna uwezekano katika miaka 20 ijayo madaktari watakuwa na uwezo wa kurudisha uhai wa wagonjwa masaa 12 hadi 24 toka wathibitishwe kufa na kuiita hiyo kuwa ni sayansi ya ufufuaji, “You could call that resurrection, if you will. But I still call it resuscitation science”.

Dr Parnia ameandika kitabu kipya kiitwacho ‘Erasing Death’.

SOURCE: DAILY MAIL

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents