Habari
‘Scorpion’ aongezewa shtaka la pili
Mkurugenzi wa mashtaka (DPP) amemuongezea shtaka lingine mshtakiwa Salumu Njwete maaarufu kama ‘Scorpion’ na sasa atakuwa akikabiliwa na mashtaka mawili Ya unyanga’nyi wa kutumia silaha na kujeruhi.
Wakili wa serikali Nassoro Katuga alimuongezea Salum shtaka hilo Jumanne hii kabla ya kusomewa shataka lake la awali, huku hakimu wa mahakama hiyo Flora Haule akiahirisha kesi hiyo hadi Disemba 14 itakaposikilizwa tena.
Mshtakiwa huyo yupo rumande kutokana na moja ya kosa linalomkabili kutokuwa na dhamana.
BY: EMMY MWAIPOPO
CHANZO: MWANANCHI