Michezo
Sebastian Nkoma ateuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara
Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania TFF limemtengaza Sebastian Nkoma kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara.
Timu hiyo inatarajia kushiriki michuano ya CECAFA ya wanawake itakayoanza Septemba 11, 2016 jijini Jinja,Uganda.
Timu hiyo imepangwa kundi B na timu za Ethiopia na Rwanda huku kundi A likiwa na timu za Uganda,Kenya,Burundi na Zanzibar.
Ni mara ya pili hii michuano hiyo kufanyika ,kwa mara ya kwanza ilifanyika Zanzibar 1986 na wenyeji kwa wakawa mabingwa.