BurudaniDiamond Platnumz

Sekeseke la Diamond

Mshindi wa tuzo ya mwanamuziki bora kwa 2010 na nyingine mbili, Diamond siku za hivi karibuni alikutana na sekeseke ambalo hatakuja kulisahau.

Diamond ambaye alikuwa akikatiza mitaa ya Ubungo bus Stand na mwanadada mmoja ambaye alikuwa amevalia nguo fupi sana ambayo ilipelekea kuacha sehemu kubwa ya mwili wake ukiwa wazi.

 

Kama ujuavyo Ubungo kulivyo na msongamano wa watu na pilikapilika na vituko vya kila siku jamaa kutokea kusikojulikana wakaibuka na kumvamia yule demu aliyekuwa na Diamond wakimshikashika na kumchania nguo yake aliyokuwa amevaa.

Alipoulizwa Diamond mwenyewe alijibu yule hakuwa demu wake bali alikuwa ni rafiki yake ambaye walikutana pale pale ubungo na kwakuwa walikuwa wanajuwana hakusita kuongea nae na ndipo sekeseke hilo lilipotokea

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents