Michezo

Sepp Blatter achunguzwa na FBI kuhusiana na hongo ya $100m

Kipindi maalumu cha uchunguzi kinachojulikana kama BBC Panorama, kimeonesha ushahidi kwamba rais wa FIFA Sepp Blatter aliyesimamishwa kwa muda, anachunguzwa na shirika la ujajusi la Marekani, FBI.

2609704800000578-0-image-a-30_1449432828803

Kuna kampuni ya masoko ya michezo inayoaminika kulipa mamilioni ya dola za Kimarekani kwa maafisa waandamizi wa FIFA katika miaka ya mwishoni mwa 1990 ili kupewa haki ya kutangaza michuano ya kombe la dunia.

Aliyekuwa ameshikia nafasi hiyo kabla ya Blatter, Joao Havelange, alikuwa ni miongoni mwa wanaotuhumiwa kupokea malipo hayo.

03CA7BA700000514-0-image-a-36_1449433058616
Joao Havelange

Blatter, amekana kuwa na taarifa yoyote ya sakata hilo, lakini kipindi cha Panorama kimeona barua iliyosainiwa na Joao Havelange ikisema Blatter ana taarifa kamili.

Source: BBC

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents