Michezo
Serena na Venus Williams waibuka na ubingwa wa pamoja Wimbledon
Madada wa Marekani, Serena na Venus Williams jana waliibuka na ubingwa wa pamoja kwenye mchezo wa tennis wakiwa pamoja Wimbledon.
Walikuwa wakichuana na Timea Babos na Yaroslavl Shvedova.
Ushindi wao ulikuwa wa seti 6-3, 6-4 katika mchezo wa saa moja na dakika 27. Ushindi huo umekuja baada ya Serena kuchukua ubingwa wa Wimbledon kwa seti 7-5, 6-3 dhidi ya Angelique Kerber.