Serengeti Fiesta Bongo movie 2011 ndani ya Dar
Tamasha la Serengeti Fiesta Filamu Bongo Movie 2011, juzi lilifikia jijini Dar es salaam katika viwanja vya Leader Club ili kutafuta watu ambao wanaweza kuigiza vizuri na wenye vipaji vya kweli, ili kuweza kuwainua na kuwa waigizaji wakubwa nchini na nje ya Nchi. Tamasha hilo ambalo lilizunguka mikoa kadhaa Tanzania, na hatmaye kurudi Dar lilipokea na wapenzi wengi wa filamu.
Majija ambao wakiongozwa na zamaradi Mtetema, walionekana kuwa makini zaidi katika kugundua kipaji cha kweli, kwa wasanii ama vikundi mbalimbali vilivyojitokeza katika kuwania nafasi hiyo pale Leader Club.
Wasanii wakionyesha uwezo wao wa kulitawala jukwaa kwa maigizo mafupi.
Wasanii wakionyesha uwezo wao, hata kuigiza kufa nayo imo.
Fundi mitambo wa Clouse Tv, nao walikuwa pamoja ilikuhakikisha kama kipindi hicho kinaenda vizuri kwenye Clouse Tv.
Wasanii wakiendeleza Mbwembwe zao
Wasanii wakisubiri zamu yao ya kuingia jukwaani kwa kuonyesha vipaji vyao.
Wasaniii wakisubiri kuitwa.