Sergio Ramos achukua jiko baada ya miaka sita ya uchumba (+Picha)
Sergio Ramos achukua jiko baada ya miaka sita ya uchumba (+Picha)
Nyota wa klabu ya Real Madrid, Sergio Ramos ameamua kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Pilar Rubio.
Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Hispania ameamua kumuoa mwanadada, Pilar Rubio ambaye ni mtangazaji wa Tv nchini Hispania baada ya kudumu naye kwa miaka sita.
Ramos ameposti picha kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram zinazoonyesha tukio hilo huku kukiwa na ujumbe unao sema kuwa ”Amesema ndiyo. Nakupenda milele.”
Mahusiano ya Ramos na mtangazaji huyo wa Tv, Rubio yalianza toka mwaka 2012. Rubio mwenye umri wa miaka 40 alikuwa ‘model’ lakini pia alishawahi kushinda tuzo ya mtangazaji bora huku miaka michache iliyopita amewahi kufanya kazi ya uchekeshaji kwenye ‘show’ iliyojulikana kama, El Hormiguero.
Mpaka sasa wawili hao wana watoto watatu watoe wakiwa wote wakiume wakati mkubwa akizaliwa mwaka 2014 na kupewa jina la Sergio na wawili wa mwisho ni Marco na Alejandro.